Posted by On the spot Tz
9:38:00 AM
0
Hassan Kessy
SIMBA SC imemsimamsha mechi tano beki wake, Hassan Ramadhani Kessy kwa kumchezea rafu isiyo ya kimchezo mshambuliaji wa Toto Africans, Edward Christopher.
Simba ilifungwa 1-0 na Toto Jumapili katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Kessy akatolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 47 kwa kumchezea rafu Edward, nyota wa zamani wa timu hiyo Msimbazi.
Pamoja na kumfungia, kocha Jackson Mayanja amewaomba radhi mashabiki wa Simba kwa matokeo hayo na kusema wanarakebisha makosa yao washinde mechi zijazo.
Abdi Banda
Mganda huyo ameshauri kikosi kisibomolewe hata kama Simba itakosa taji msimu huu, ili kiboreshwe na msimu ujao kirejee na nguvu mpya.
Kuhusu kiungo Abdi Banda, kocha huyo amesema mchezaji huyo hajafukuzwa bali amejiondoa mwenyewe kwenye timu baada ya kususa.
Baada ya kupoteza mchezo na Toto kwa bao pekee la Waziri Junior dakika ya 20, Simba inabaki na pointi zake 57 baada ya kucheza mechi 25, ikiendelea kuwa nafasi ya pili, mbele ya Azam FC yenye pointi 55 za mechi 24, wakati Yanga wenye pointi 59 za mechi 24 wapo juu yao.
Wakati huo huo: Simba SC inatarajiwa kuingia kambini visiwani Zanzibar Ijumaa kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Azam FC Mei 1, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
onthespotz.blogspot.com
SIMBA SC imemsimamsha mechi tano beki wake, Hassan Ramadhani Kessy kwa kumchezea rafu isiyo ya kimchezo mshambuliaji wa Toto Africans, Edward Christopher.
Simba ilifungwa 1-0 na Toto Jumapili katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Kessy akatolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 47 kwa kumchezea rafu Edward, nyota wa zamani wa timu hiyo Msimbazi.
Pamoja na kumfungia, kocha Jackson Mayanja amewaomba radhi mashabiki wa Simba kwa matokeo hayo na kusema wanarakebisha makosa yao washinde mechi zijazo.
Abdi Banda
Mganda huyo ameshauri kikosi kisibomolewe hata kama Simba itakosa taji msimu huu, ili kiboreshwe na msimu ujao kirejee na nguvu mpya.
Kuhusu kiungo Abdi Banda, kocha huyo amesema mchezaji huyo hajafukuzwa bali amejiondoa mwenyewe kwenye timu baada ya kususa.
Baada ya kupoteza mchezo na Toto kwa bao pekee la Waziri Junior dakika ya 20, Simba inabaki na pointi zake 57 baada ya kucheza mechi 25, ikiendelea kuwa nafasi ya pili, mbele ya Azam FC yenye pointi 55 za mechi 24, wakati Yanga wenye pointi 59 za mechi 24 wapo juu yao.
Wakati huo huo: Simba SC inatarajiwa kuingia kambini visiwani Zanzibar Ijumaa kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Azam FC Mei 1, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
onthespotz.blogspot.com

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: