
Posted by On the spot Tz
9:23:00 AM
0
Baraza Wazee wa Yanga wameshtukia hujuma ndani ya klabu hiyo, baada ya kugundua kuwepo watu wanaotumika kutaka kuivuruga timu hiyo katika kuelekea uchaguzi mkuu.
Kauli hiyo, imetolewa na wazee wa timu hiyo leo kwenye Makao Makuu ya timu hiyo yaliyopo mitaa ya Jangwani na Twiga jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Baraza hilo, Ibrahim Omary Akilimali amesema wanachama wa timu hiyo hawatakiwi kuyumbishwa na baadhi ya wanachama wanaochukia mafanikio ya mwenyekiti wao Yusuf Manji kutokana na mafanikio wanayoyapata.
Akilimali alisema, baadhi ya wanachama hao wanatumika kumchafua mwenyekiti wao kwenye vyombo vya habari kwa lengo la kuivuruga timu kimakusudi.
“Jana wameona umati mkubwa wa mashabiki waliojitokeza kwenye mapokezi ya timu yetu Uwanja wa Ndege baada vijana wetu kuiwezesha timu yetu kufuzu hatua ya makundi ya nane bora kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.
“Baada ya kuona umati huo, leo asubuhi tumeona moja ya magazeti likimuandika vibaya mwenyekiti wetu, sasa walikuwa wapi siku kumuandika vibaya hadi walipoona timu yetu imefuzu hatua ya makundi, hivyo ninawatahadharisha wanachama kuachana na maneno hayo,”alisema Akilimali.
"Tunajua hizi njama za kuona Yanga inafeli, ikifanikiwa inawaumiza baadhi ya watu ambao wanataka kuonekana wao ndio wana mafanikio zaidi.
"Wakati fulani tulikuwa nao hapa Yanga lakino hakukuwa na mafanikio yoyote. Sasa wanaona mafanikio ya Yanga kama yanawaumiza wao. Watuache tuendelee kupambana.
"Kama wataendelea hivi itafikia hatua tutatangaza uadui kati yao na sisi, tutatangaza watu waachane kabisa na bidhaa zao."
Hata hivyo, mzee Akilimali hakutaka kutaja jina la mhusika anayewashambulia.
"Tunajua hizi njama za kuona Yanga inafeli, ikifanikiwa inawaumiza baadhi ya watu ambao wanataka kuonekana wao ndio wana mafanikio zaidi.
"Wakati fulani tulikuwa nao hapa Yanga lakino hakukuwa na mafanikio yoyote. Sasa wanaona mafanikio ya Yanga kama yanawaumiza wao. Watuache tuendelee kupambana.
"Kama wataendelea hivi itafikia hatua tutatangaza uadui kati yao na sisi, tutatangaza watu waachane kabisa na bidhaa zao."
Hata hivyo, mzee Akilimali hakutaka kutaja jina la mhusika anayewashambulia.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: