Posted by On the spot Tz
10:59:00 PM
0
Klabu ya Azam, jana Jumanne imezindua duka la vifaa vya michezo ambapo litakuwa likiuza bidhaa zenye nembo ya klabu hiyo pekee.
Miongoni mwa bidhaa ambazo zitakuwa zikipatikana katika duka hilo lililopo kwenye makutano ya mitaa ya Swahili na Mkunguni, Kariakoo jijini Dar, ni pamoja na jezi, soksi, mabegi na kofia.
Baada ya kuzindua duka hilo, Mtendaji Mkuu wa Azam, Saad Kawemba, amesema: “Huu ni mwanzo tu, tutafungua maduka mengine katika sehemu mbalimbali za jiji hili na mikoani lengo likiwa ni kuitangaza nembo yetu.”
Kawemba aliongeza kuwa, duka hilo litakuwa likifunguliwa kila siku kuanzia saa 2:30 asubuhi na kufungwa saa 2:30 usiku ambapo muda huo utatoa fursa kwa kila mmoja kwa nafasi yake kufika dukani hapo na kujipatia bidhaa za klabu yao ya Azam.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: