Posted by On the spot Tz
1:08:00 PM
0
Licha ya kupoteza mchezo wa jana dhidi ya Nigeria, Taifa Stars wamevuna kitita cha dola 10,000 kutoka kwa Gavana wa jimbo la Akwa Ibom State, Udom ambapo ndipo unapopatikana Uwanja wa Uyo uliotumika kwenye mchezo wa jana.
Kitita hicho ni sawa na shilingi za Kitanzania ml 21.7 na Gavana huyo alitoa wakati waliokuwa wakipata chakula cha usiku kwa pamoja baada ya mchezo huo.
Ikumbukwe kuwa katika historia ya timu hizi mbili, Tanzania haijawahi kuifunga Nigeria katika michezo yote waliyowahi kukutana zaidi ya kuambulia vichapo na sare.
Gavana huyo ametoa kiasi hicho cha fedha kutokana na ari ya upiganaji iliyooneshwa na wachezaji wa Stars, ambao walikuwa wakiongozwa na nahodha wao Mbwana Samatta ambaye kabla ya mchezo huo alikuwa gumzo kwa Wanigeria.
Hata hivyo, jana kuna wachezaji ambao walionesha kiwango kikubwa sana kilichowapa mashaka Nigeria. Wachezaji hao ni pamoja na Aishi Manula, Simon Msuva na mabeki wa kati Vincent Andew na David Mwantika.
Vilevile Gavana huyo pia aliwapa Nigeria Naira mil 10 kama pongezi kwa ushindi wao waliopata na kuahidi kuwapa zaidi endapo watafanikiwa kupata nafasi ya kushiriki fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Russia.
Kitita hicho ni sawa na shilingi za Kitanzania ml 21.7 na Gavana huyo alitoa wakati waliokuwa wakipata chakula cha usiku kwa pamoja baada ya mchezo huo.
Ikumbukwe kuwa katika historia ya timu hizi mbili, Tanzania haijawahi kuifunga Nigeria katika michezo yote waliyowahi kukutana zaidi ya kuambulia vichapo na sare.
Gavana huyo ametoa kiasi hicho cha fedha kutokana na ari ya upiganaji iliyooneshwa na wachezaji wa Stars, ambao walikuwa wakiongozwa na nahodha wao Mbwana Samatta ambaye kabla ya mchezo huo alikuwa gumzo kwa Wanigeria.
Hata hivyo, jana kuna wachezaji ambao walionesha kiwango kikubwa sana kilichowapa mashaka Nigeria. Wachezaji hao ni pamoja na Aishi Manula, Simon Msuva na mabeki wa kati Vincent Andew na David Mwantika.
Vilevile Gavana huyo pia aliwapa Nigeria Naira mil 10 kama pongezi kwa ushindi wao waliopata na kuahidi kuwapa zaidi endapo watafanikiwa kupata nafasi ya kushiriki fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Russia.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Shilingi Bilioni 3 na Mali za Bilioni 10 zataifishwa na TRA Kutoka kwa Wakwepa Kodi Bandari Kavu ya Azam,,,,,,,Mamlaka ya kukusanya kodi TRA kupitia madalali wa Yono Auction Mart wamekusanya mali za bilioni 3 pamoja na kutaifisha mali za b...



No comments: