Posted by On the spot Tz
2:49:00 PM
0
Mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe amefunguka na kujibu kauli ambayo
ametoa Rais Magufuli kuvitaka vyama vya siasa kuacha kufanya siasa mpaka
kipindi cha kampeni tena katika uchaguzi wa mwaka 2020.
Zitto Kabwe ametumia ukurasa wake wa facebook kujibu kauli hiyo kwa kuonyesha kusikitishwa huku na kusema kauli hiyo wao kama wazalendo wanaichukulia kama ni vita dhidi ya demokrasia.
"Tumepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa kauli ya Rais kwamba vyama vya siasa havipaswi kufanya siasa isipokuwa wakati wa Kampeni na kupitia bungeni. Tunaichukulia kauli ya Rais Kama tangazo la vita dhidi ya demokrasia na uhai wa vyama vingi nchini. Chama chetu kitaitisha vikao vya dharura kujadili hali ya nchi na namna ya kukabiliana na mashambulizi yanayoendelea dhidi ya demokrasia nchini mwetu". Aliandika Zitto Kabwe
Mbali na hilo Mbunge huyo aliwataka wanasiasa pamoja na vyama vya siasa kuungana pamoja sasa katika vita hii dhidi ya demokrasia na kuacha tofauti zao ili kuweza kufikia lengo hilo.
"Tunatoa wito kwa Vyama vyote vya siasa nchini kuunganisha nguvu katika kuhakikisha tunapigana vita hii pamoja. Huu ni wakati wa vyama vya siasa na wanasiasa kuacha tofauti zao na kupambana kulinda uhuru wa kufanya siasa wakati wowote kwa mujibu wa Sheria. Tunatoa wito Kwa wananchi wote na taasisi za kiraia kusimama imara Katika Kulinda demokrasia. Tunasisitiza kuwa ushahidi wa kisayansi unaonyesha kuwa huwezi kuua demokrasia bila kuua juhudi za maendeleo. Tusiruhusu mtu yeyote mwenye mamlaka kuua demokrasia nchini mwetu". Alisisitiza Zitto Kabwe
onthespottz.blogspot.com
Zitto Kabwe ametumia ukurasa wake wa facebook kujibu kauli hiyo kwa kuonyesha kusikitishwa huku na kusema kauli hiyo wao kama wazalendo wanaichukulia kama ni vita dhidi ya demokrasia.
"Tumepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa kauli ya Rais kwamba vyama vya siasa havipaswi kufanya siasa isipokuwa wakati wa Kampeni na kupitia bungeni. Tunaichukulia kauli ya Rais Kama tangazo la vita dhidi ya demokrasia na uhai wa vyama vingi nchini. Chama chetu kitaitisha vikao vya dharura kujadili hali ya nchi na namna ya kukabiliana na mashambulizi yanayoendelea dhidi ya demokrasia nchini mwetu". Aliandika Zitto Kabwe
Mbali na hilo Mbunge huyo aliwataka wanasiasa pamoja na vyama vya siasa kuungana pamoja sasa katika vita hii dhidi ya demokrasia na kuacha tofauti zao ili kuweza kufikia lengo hilo.
"Tunatoa wito kwa Vyama vyote vya siasa nchini kuunganisha nguvu katika kuhakikisha tunapigana vita hii pamoja. Huu ni wakati wa vyama vya siasa na wanasiasa kuacha tofauti zao na kupambana kulinda uhuru wa kufanya siasa wakati wowote kwa mujibu wa Sheria. Tunatoa wito Kwa wananchi wote na taasisi za kiraia kusimama imara Katika Kulinda demokrasia. Tunasisitiza kuwa ushahidi wa kisayansi unaonyesha kuwa huwezi kuua demokrasia bila kuua juhudi za maendeleo. Tusiruhusu mtu yeyote mwenye mamlaka kuua demokrasia nchini mwetu". Alisisitiza Zitto Kabwe
onthespottz.blogspot.com
Tagged with:
HABARI KITAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...



No comments: