Posted by On the spot Tz
3:07:00 PM
0
| RAIS WA TFF, JAMAL MALINZI NA RAIS WA CAF, ISSA HAYATOU WAKIWA PAMOJA |
Shirikisho
la Soka Tanzania (TFF), limepokea taarifa juu ya mpango na kauli za
baadhi ya viongozi wa Young Africans SC kushawishi mashabiki wao kufanya
vurugu dhidi ya warushaji matangazo ya televisheni ya moja kwa moja
wakati wa mchezo wa Kombe la Shirikisho la Afrika ngazi ya Makundi kati
ya Young Africans ya Tanzania na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo (DRC) utakaofanyika Juni 28, 2016 saa 10.00 jioni kwenye Uwanja
wa Dar es Salaam.
TFF
ikiwa msimamizi mkuu wa mpira wa miguu Tanzania, inawajibika na mara
moja inachukua nafasi hii kuwatahadharisha baadhi ya viongozi wa Young
Africans, wanachama na mashabiki wao kutofanya hivyo kwani itakuwa ni
kinyume na kanuni za mashindano na mikataba ya udhamini katika hatua
hii.
Ikumbukwe
kwamba CAF inamiliki asilimia mia moja ya haki za habari na masoko
katika ngazi hii ya makundi na jaribio lolote la kukwamisha matangazo ya
biashara au utengenezaji na urushaji wa matangazo ya televisheni au
ukwamishaji wa shughuli zingine kama hizo kwa CAF au wakala aliyeteuliwa
na CAF kutaigharimu klabu mwenyeji si kwa kutozwa faini tu lakini pia
uwezekano wa kuondolewa mashindanoni.
Pia
TFF inatoa tahadhari hiyo ikiwamo ile ya utamaduni wa kukaa uwanjani
ili kuepusha aina yoyote ya vurugu kwenye michezo yake hususani hii ya
hatua ya makundi. TFF inafahamu kuwa tayari viongozi wa Young Africans
walikwisha kusoma nyaraka na taarifa mbalimbali kuhusu kanuni na masuala
ya udhamini kwa timu zinazofuzu hatua ya Nane Bora.Wapenzi wa Yanga
wanaombwa kufika kwa wingi na kuishangilia kwa nguvu timu yao ikiwa ni
njia ya kuitia hamasa.Hata hivyo shamrashamra hizo zifanyike kwa kufuata
sheria,kanuni na taratibu za Mpira wa Miguu na sheria za nchi.
Vitendo
vya kuashiria vurugu na kufanya vurugu vikithibitishwa katika taarifa
ya Mwamuzi, Janny Sikazwe wa Zambia; Kamishna wa mchezo, Celestin
Ntangungira wa Rwanda na Mratibu Mkuu Maalumu kutoka Msumbiji, Sidio
Jose Mugadza, hatua zake zitachukuliwa dhidi yake ikiwamo KUONDOLEWA KWENYE MASHINDANO. Vilevile vitendo vya kutishia amani,kudhuru mwili au kuharibu mali vitachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za kijinai.
Katika
mchezo huo wa kimataifa Na. 107, Mwamuzi Sikazwe atasaidiwa na Jarson
Emiliano dos Santos kutoka Angola atayekuwa kwenye mstari wa kulia (line
1) na Berhe O’Michael wa Eritrea atayekuwa upande wa kushoto (line 2)
huku Wellington Kaoma wa Zambia akiwa ni mwamuzi wa akiba.
Wakati huohuo, kikao
cha Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini
kinatarajia kukaa siku ya Jumamosi tarehe 2 Julai 2016. Taarifa zaidi
itatolewa karibuni.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: