Posted by On the spot Tz
9:27:00 AM
0
Sasa ni siku chache tu baada ya Yanga kufanikiwa kumsajili, Obrey Chirwa raia wa Zambia, mpachika mabao wa timu hiyo, raia wa Burundi, Amissi Tambwe, amedai kuwa hana wasiwasi na ujio wa nyota huyo kikosini hapo.
Yanga imemleta Chirwa kutoka FC Platinum ya Zimbabwe ili kuimarisha safu yake ya ushambuliaji.
Tambwe ambaye ni mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita baada ya kupiga mabao 21, amesema anajiamini na ana uhakika wa kubakia katika kikosi cha kwanza cha Yanga endapo kocha mkuu wa timu hiyo, Mholanzi, Hans van Der Pluijm atapenda.
“Sina wasiwasi na nafasi yangu kwani najiamini na Mungu akipenda nitaendelea kuwa kikosi cha kwanza na nitazidi kufanya vizuri kama ilivyokuwa msimu uliopita.
“Naongea hivyo kwa sababu najiamini na ninajua nini ninachokifanya, kwa hiyo sihofii mchezaji yeyote ila nawapongeza Yanga kwa usajili wa Chirwa kwani tunachotaka sisi ni mafanikio, hivyo nitashirikiana naye kwa kila jambo kama nilivyokuwa nikishirikiana na (Donald) Ngoma,” alisema Tambwe.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
WATOTO WA KAGAME WAITIKISA TIMU YA TAIFA YA RWANDA,,,,,,Kwa mara ya Kwanza wanawe rais wa Rwanda Paul Kagame, Bryan Kagame na Ian Kagame waliiwakilisha timu ya taifa ya Rwanda kwa wachezaji wasi...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: