Posted by On the spot Tz
9:27:00 AM
0
Sasa ni siku chache tu baada ya Yanga kufanikiwa kumsajili, Obrey Chirwa raia wa Zambia, mpachika mabao wa timu hiyo, raia wa Burundi, Amissi Tambwe, amedai kuwa hana wasiwasi na ujio wa nyota huyo kikosini hapo.
Yanga imemleta Chirwa kutoka FC Platinum ya Zimbabwe ili kuimarisha safu yake ya ushambuliaji.
Tambwe ambaye ni mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita baada ya kupiga mabao 21, amesema anajiamini na ana uhakika wa kubakia katika kikosi cha kwanza cha Yanga endapo kocha mkuu wa timu hiyo, Mholanzi, Hans van Der Pluijm atapenda.
“Sina wasiwasi na nafasi yangu kwani najiamini na Mungu akipenda nitaendelea kuwa kikosi cha kwanza na nitazidi kufanya vizuri kama ilivyokuwa msimu uliopita.
“Naongea hivyo kwa sababu najiamini na ninajua nini ninachokifanya, kwa hiyo sihofii mchezaji yeyote ila nawapongeza Yanga kwa usajili wa Chirwa kwani tunachotaka sisi ni mafanikio, hivyo nitashirikiana naye kwa kila jambo kama nilivyokuwa nikishirikiana na (Donald) Ngoma,” alisema Tambwe.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...



No comments: