Posted by On the spot Tz
2:32:00 PM
0
Mwanafunzi wa chekechea shule ya msingi Ilunga amefariki dunia baada ya kupigwa fimbo na baba yake wa kambo wilayani Magu mkoani Mwanza.
Taarifa ya jeshi la polisi imeeleza kuwa mnamo tarehe 27.06.2016 majira ya saa 12:00 jioni katika kitongoji cha Moha kijiji cha Ilungu kata ya Nyigogo tarafa ya Itumbili wilaya ya Magu mkoani Mwanza, mtoto aliyejulikana kwa jina la Julius Leonard miaka [7] mwanafunzi wa chekechea shule ya msingi ilunga aliuawa kwa kupigwa fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake na baba yake wa kambo aitwaye Leonard Joseph miaka [32] mkulima na mkazi wa kijiji cha Ilunga.
Inadaiwa kuwa marehemu alitumwa na baba yake huyo wa kambo kwenda kuchukua betrii ya simu iliyokuwa imepelekwa kuchajiwa ndipo alichelewa kurudi nyumbani hali iliyopelekea baba yake huyo kuwa na hasira na kuamua kumchapa hadi mtoto huyo akapoteza maisha.
Mwili wa marehemu tayari umefanyiwa uchunguzi wa awali na daktari na kuonekana ukiwa na alama za fimbo huku mguu wa kushoto ukionekana kuvuja damu kwa ndani kutokana na adhabu ya fimbo hizo.
Mtuhumiwa wa mauaji hayo ametoroka baada ya kuona amefanya mauaji.
Jeshi la polisi linaendelea na upelelezi pamoja na uchunguzi kuhusiana natukio hilo, huku msako wa kumsaka na kumtia nguvuni mtuhumiwa wa mauaji tajwa hapo juu ukiwa unaendelea.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi Ahmed Msangi anatoa wito kwa wananchi akiwataka kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi, kwa kutoa taarifa za mtuhumiwa wa mauaji haya mahali alipo ili awezwe kukamatwa na kufikishwa.
onthespottz.blogspot.com
Taarifa ya jeshi la polisi imeeleza kuwa mnamo tarehe 27.06.2016 majira ya saa 12:00 jioni katika kitongoji cha Moha kijiji cha Ilungu kata ya Nyigogo tarafa ya Itumbili wilaya ya Magu mkoani Mwanza, mtoto aliyejulikana kwa jina la Julius Leonard miaka [7] mwanafunzi wa chekechea shule ya msingi ilunga aliuawa kwa kupigwa fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake na baba yake wa kambo aitwaye Leonard Joseph miaka [32] mkulima na mkazi wa kijiji cha Ilunga.
Inadaiwa kuwa marehemu alitumwa na baba yake huyo wa kambo kwenda kuchukua betrii ya simu iliyokuwa imepelekwa kuchajiwa ndipo alichelewa kurudi nyumbani hali iliyopelekea baba yake huyo kuwa na hasira na kuamua kumchapa hadi mtoto huyo akapoteza maisha.
Mwili wa marehemu tayari umefanyiwa uchunguzi wa awali na daktari na kuonekana ukiwa na alama za fimbo huku mguu wa kushoto ukionekana kuvuja damu kwa ndani kutokana na adhabu ya fimbo hizo.
Mtuhumiwa wa mauaji hayo ametoroka baada ya kuona amefanya mauaji.
Jeshi la polisi linaendelea na upelelezi pamoja na uchunguzi kuhusiana natukio hilo, huku msako wa kumsaka na kumtia nguvuni mtuhumiwa wa mauaji tajwa hapo juu ukiwa unaendelea.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi Ahmed Msangi anatoa wito kwa wananchi akiwataka kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi, kwa kutoa taarifa za mtuhumiwa wa mauaji haya mahali alipo ili awezwe kukamatwa na kufikishwa.
onthespottz.blogspot.com
Tagged with:
HABARI KITAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...



No comments: