Posted by On the spot Tz
9:23:00 AM
0
Siku moja baada ya wakili wa Askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, Peter Kibatala kuwaandikia barua Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamanda Simon Sirro amesema hawafanyi kazi kwa kufuata barua ya askofu huyo.
Sirro alithibitisha kupata barua hiyo, lakini akasema kuwa wanaendelea kumtafuta popote pale alipo na wakifahamu watamtia nguvuni.
Sakata la kutafutwa kwa kiongozi huyo linazidi kushika kasi kutokana na sintofahamu ya kubaini alipo, ikiwamo kambi ya muda wa saa saba iliyowekwa na polisi nyumbani kwa Gwajima, ambayo haikuwa na mafanikio wiki iliyopita.
Baada ya sintofahamu ya wiki nzima huku kukiwa na uvumi kuwa yupo nje ya nchi na wengine wakidai yupo nchini, juzi wakili Kibatala aliwasilisha barua Polisi akidai mteja wake yupo nje ya nchi na aliposafiri hakuwa anajua kama anatafutwa na polisi.
Katika barua hiyo Kibatala alisema ameelekezwa na mteja wake kufikisha ujumbe huo na akirejea atajisalimisha polisi kuitikia wito huo.
Jana Kibatala alisisitiza kuwa: “Kwa sasa yupo nje ya nchi akihubiri injili, alisafiri kabla ya kupata taarifa kuwa anatafutwa na polisi ana mashauri katika Mahakama ya Kisutu Julai Mosi, hivyo kabla ya hapo atakuwa amesharejea.”
Lakini Sirro alisema barua hiyo ni kujitetea ambako hakuna maana na wanachofanya wao ni kuendelea kumtafuta badala ya kusubiri ajisalimishe kama ulivyoandikwa waraka huo.
“Suala la kutupa taarifa za kujifanya alikuwa hafahamu kama anatafutwa si kweli, tukifahamu mahali alipo hata sasa hivi tunakwenda kumkamata, hatufanyi kazi kwa kufuata maelekezo yake,” alisema Kamanda Sirro.
Sirro alifafanua kuwa bado wanafuatilia kubaini kama yupo nchini au nje ya nchi, wakitambua ni nje nchi atakamatwa huko huko kwa msaada wa Interpol.
“Hatujafahamu alipo hata huko nje Interpol wapo kuwashughulikia watu kama hawa wanaofanya ukorofi nchini na kukimbilia nje ya nchi wakidhani wanatatua tatizo, kumbe wanaliahirisha,” alisema Sirro.
onthespottz.blogspot.com
Sirro alithibitisha kupata barua hiyo, lakini akasema kuwa wanaendelea kumtafuta popote pale alipo na wakifahamu watamtia nguvuni.
Sakata la kutafutwa kwa kiongozi huyo linazidi kushika kasi kutokana na sintofahamu ya kubaini alipo, ikiwamo kambi ya muda wa saa saba iliyowekwa na polisi nyumbani kwa Gwajima, ambayo haikuwa na mafanikio wiki iliyopita.
Baada ya sintofahamu ya wiki nzima huku kukiwa na uvumi kuwa yupo nje ya nchi na wengine wakidai yupo nchini, juzi wakili Kibatala aliwasilisha barua Polisi akidai mteja wake yupo nje ya nchi na aliposafiri hakuwa anajua kama anatafutwa na polisi.
Katika barua hiyo Kibatala alisema ameelekezwa na mteja wake kufikisha ujumbe huo na akirejea atajisalimisha polisi kuitikia wito huo.
Jana Kibatala alisisitiza kuwa: “Kwa sasa yupo nje ya nchi akihubiri injili, alisafiri kabla ya kupata taarifa kuwa anatafutwa na polisi ana mashauri katika Mahakama ya Kisutu Julai Mosi, hivyo kabla ya hapo atakuwa amesharejea.”
Lakini Sirro alisema barua hiyo ni kujitetea ambako hakuna maana na wanachofanya wao ni kuendelea kumtafuta badala ya kusubiri ajisalimishe kama ulivyoandikwa waraka huo.
“Suala la kutupa taarifa za kujifanya alikuwa hafahamu kama anatafutwa si kweli, tukifahamu mahali alipo hata sasa hivi tunakwenda kumkamata, hatufanyi kazi kwa kufuata maelekezo yake,” alisema Kamanda Sirro.
Sirro alifafanua kuwa bado wanafuatilia kubaini kama yupo nchini au nje ya nchi, wakitambua ni nje nchi atakamatwa huko huko kwa msaada wa Interpol.
“Hatujafahamu alipo hata huko nje Interpol wapo kuwashughulikia watu kama hawa wanaofanya ukorofi nchini na kukimbilia nje ya nchi wakidhani wanatatua tatizo, kumbe wanaliahirisha,” alisema Sirro.
onthespottz.blogspot.com
Tagged with:
HABARI KITAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...



No comments: