Posted by On the spot Tz
1:50:00 PM
0
Watu wanane wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika shambulio lililofanywa msikitini na watu waliokuwa na silaha katika mji wa al Junaynah mkoani Darfur Magharibi huko Sudan.
Shirika la habari la kimataifa la Qurani (Iqna) limeripoti leo kuwa shambulizi hilo lililofanywa na kundi la watu wenye silaha katika eneo la Azaran karibu na mji wa al Junaynah limetajwa kuwa ni shambulio la kulipiza kisasi.
Kufuatia shambulio hilo, maafisa husika wa mkoa wa Darfur wamezidisha idadi ya wanajeshi kutokana na kuweko uwezekano wa kufanyika maandamano ya wananchi na kusababisha ghasia mitaani.
Hii ni katika hali ambayo mizozo ya kikabila katika mji wa al Junaynah imesababisha hali ya wasiwasi miongoni mwa wakazi wa mji huo na viongozi wa mji huo huko Darfur Magharibi. Hadi kufikia sasa jitihada rasmi za kumaliza mizozo hiyo ya kikabila zimegonga mwamba na inasemekana kuwa hali hiyo imekuwa na taathira hasi kwa muundo wa kijamii wa mji huo. Aidha kuongeza ghasia na mashambulizi chungu nzima katika mji wa al Junaynah kunasababishwa na mambo mengi tu moja ikiwa ni kukosekana udhibiti na usimamizi mzuri wa hali ya usalama na makundi yanayobeba silaha, masuala yanayorahisisha upatikanaji silaha kwa makabila yanayozozana.

Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: