
Posted by On the spot Tz
1:38:00 AM
0
WATUHUMIWA wawili Zuberi Thabiti (30) na Iddy Adamu (32) wanaodaiwa kushirikiana kufanikisha tukio la kumbaka na kumdhalilisha binti mkulima (jina limehifadhiwa), mkazi wa Kata ya Dakawa, wilayani Mvomero, mkoani Morogoro, wamekatwa na kohojiwa na jeshi la polisi mkoani humo.
Watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya tukio hilo la kinyama usiku wa Mei 4, mwaka huu katika nyumba ya kulala wageni iitwayo Titii iliyoko Dakawa ambapo Zuberi aambaye ni dereva, mkazi wa Mbarali Mbeya anadaiwa kumbaka binti huyo huku Iddy ambaye ni mkulima, mkazi wa Makambako akirekodi picha za video kwa kutumia simu yake ya mkononi.
Kwa mujibu wa taarifa ya polisi, baada ya kurekodi katika simu yake, baadaye Iddy alizituma picha hizo kwa mtu aliyefahamika kwa jina la Rajabu Salehe (26), mkazi wa Dakawa ambaye naye alizisambaza picha hizo katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwa watu mbalimbali.
Taarifa ya polisi imeeleza kuwa, chanzo cha tukio hilo ni kwamba, binti huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Zuberi ambapo siku hiyo mtuhumiwa alimpigia simu binti huyo na kumwambia aende katika nyumba hiyo ya wageni.
Taarifa hiyo ya polisi imezidi kueleza kuwa, baada ya kufika katika chumba husika ndipo Iddy alipoingia kisha kumtaka binti huyo afanye atakachomuelekeza huku akimshikia kisu ili asipige kelele na baada ya kutekeleza ukatili huo (ubakaji), walimtaka asitoe siri hiyo vinginevyo atauawa.
Aidha, baada ya tukio hilo kuripotiwa kituo cha Polisi Dakawa Apliri 5, mwaka huu, polisi walianza uchunguzi mara moja ambapo walifanikiwa kuwakamata jumla ya watuhumiwa 11 wakiwemo Zuberi na Iddy pamoja na walioshiriki kuzisambaza picha hizo za udhalilishaji ambao ni;
Rajabu Salehe (26), Saidi Athumani (26), Musini Ngai (36), Saidi Mohamedi (24), John Peter (24), Hassani Ramadhani (27), Ramadhani Ally (26), Lulu Peter (38) na Magreth Njonjome (30), wote wakazi wa Dakawa ambapo kwa pamoja wamefunguliwa shitaka la PICHA ZA UTUPU (PONOGRAFIA) chini ya kifungu cha 14 (1) (a) cha sheria ya makosa ya mtandao.
Taarifa hiyo ya polisi pia imeeleza kuwa jeshi hilo linaendelea kuwatafuta watuhumiwa wengine huku jeshi hilo likitoa onyo kwa wananchi wote kuwa makini na matumizi ya mitandao ya kijamii kwa kutoshiriki makosa ya uhalifu wa kimtandao kwani sheria itachukua mkondo wake.
Katika hatua nyingine, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu leo alikemea suala hilo bungeni na kueleza masikitiko yake makubwa kwa watu hao kutekeleza unyama huo na kusisitiza kuwa watuhumiwa hao wafikishwe mahakamani haraka.
onthespottz.blogspot.com
Watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya tukio hilo la kinyama usiku wa Mei 4, mwaka huu katika nyumba ya kulala wageni iitwayo Titii iliyoko Dakawa ambapo Zuberi aambaye ni dereva, mkazi wa Mbarali Mbeya anadaiwa kumbaka binti huyo huku Iddy ambaye ni mkulima, mkazi wa Makambako akirekodi picha za video kwa kutumia simu yake ya mkononi.
Kwa mujibu wa taarifa ya polisi, baada ya kurekodi katika simu yake, baadaye Iddy alizituma picha hizo kwa mtu aliyefahamika kwa jina la Rajabu Salehe (26), mkazi wa Dakawa ambaye naye alizisambaza picha hizo katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwa watu mbalimbali.
Taarifa ya polisi imeeleza kuwa, chanzo cha tukio hilo ni kwamba, binti huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Zuberi ambapo siku hiyo mtuhumiwa alimpigia simu binti huyo na kumwambia aende katika nyumba hiyo ya wageni.
Taarifa hiyo ya polisi imezidi kueleza kuwa, baada ya kufika katika chumba husika ndipo Iddy alipoingia kisha kumtaka binti huyo afanye atakachomuelekeza huku akimshikia kisu ili asipige kelele na baada ya kutekeleza ukatili huo (ubakaji), walimtaka asitoe siri hiyo vinginevyo atauawa.
Aidha, baada ya tukio hilo kuripotiwa kituo cha Polisi Dakawa Apliri 5, mwaka huu, polisi walianza uchunguzi mara moja ambapo walifanikiwa kuwakamata jumla ya watuhumiwa 11 wakiwemo Zuberi na Iddy pamoja na walioshiriki kuzisambaza picha hizo za udhalilishaji ambao ni;
Rajabu Salehe (26), Saidi Athumani (26), Musini Ngai (36), Saidi Mohamedi (24), John Peter (24), Hassani Ramadhani (27), Ramadhani Ally (26), Lulu Peter (38) na Magreth Njonjome (30), wote wakazi wa Dakawa ambapo kwa pamoja wamefunguliwa shitaka la PICHA ZA UTUPU (PONOGRAFIA) chini ya kifungu cha 14 (1) (a) cha sheria ya makosa ya mtandao.
Taarifa hiyo ya polisi pia imeeleza kuwa jeshi hilo linaendelea kuwatafuta watuhumiwa wengine huku jeshi hilo likitoa onyo kwa wananchi wote kuwa makini na matumizi ya mitandao ya kijamii kwa kutoshiriki makosa ya uhalifu wa kimtandao kwani sheria itachukua mkondo wake.
Katika hatua nyingine, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu leo alikemea suala hilo bungeni na kueleza masikitiko yake makubwa kwa watu hao kutekeleza unyama huo na kusisitiza kuwa watuhumiwa hao wafikishwe mahakamani haraka.
onthespottz.blogspot.com

Tagged with:
HABARI KITAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
WATOTO WA KAGAME WAITIKISA TIMU YA TAIFA YA RWANDA,,,,,,Kwa mara ya Kwanza wanawe rais wa Rwanda Paul Kagame, Bryan Kagame na Ian Kagame waliiwakilisha timu ya taifa ya Rwanda kwa wachezaji wasi...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: