Posted by On the spot Tz
12:11:00 PM
0
KOCHA Mkuu wa Yanga SC, Hans van der Pluijm amewaacha wachezaji wanne katika safari ya Angola asubuhi ya kesho kwa sababu mbalimbali.
Hao ni kipa Benedicto Tinocco ambaye hayumo kwenye programu za mchezo sawa na viungo Said Juma na Issoufou Boubacar, wakati Malimi Busungu ni majeruhi.
Yanga inatarajiwa kuondoka Saa 12:00 asubuhi ya kesho kwenda Angola kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa mchujo wa kuwania kutinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji Sagrada Esperanca Jumatano.
Katika mchezo huo, Yanga itahitaji hata sare kusonga mbele, baada ya awali kushinda 2-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, mabao ya Simon Msuva na Matheo Anthony.
Mechi hiyo itachezeshwa na marefa wa Madagascar, Hamada el Moussa Nampiandraza atakayepuliza filimbi, akisaidiwa na washika vibendera Velomanana Ferdinand Jinoro na Jean Thierry Djaonirina.
Yanga imeangukia katika kapu la kuwania kucheza hatua ya makundi ya Shirikisho, baada ya kutolewa na Al Ahly ya Misri katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao 3-2, ikilazimishwa sare ya 1-1 Dar es Salaam na kufungwa 2-1 Alexandria.
Yanga ilianza vizuri tu kwa kuzitoa Cercle de Joachim ya Mauritius kwa jumla ya mabao 3-0, ikishinda 1-0 ugenini na 2-0 nyumbani kabla ya kuitoa na APR ya Rwanda kwa jumla ya mabao 3-2, ikishinda 2-1 Kigali na kutoa sare ya 1-1 Dar es Salaam.
Kwa upande wao, Sagrada Esperanca katika Raundi ya Awali waliitoa Ajax Cape Town ya Afrika Kusini kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya kufungwa 2-1 ugenini na kushinda 2-0 nyumbani. Katika Raundi ya kwanza wakaitoa LD Maputo ya Msumbiji kwa jumla ya mabao 2-1 ikishinda 1-0 nyumbani na kutoa sare ya 1-1 ugenini na kwenda hatua ya 16 Bora, ambako waliitoa V. Club Mokanda ya Kongo kwa jumla ya mabao 4-1 wakishinda 2-1 ugenini na 2-0 nyumbani.
Kila la heri na safari njema Yanga SC.
KIKOSI CHA YANGA KILICHOPO KIGALI;
Makipa; Ally Mustafa ‘Barthez’ na Deo Munishi ‘Dida’.
Mabeki; Juma Abdul, Mwinyi Haji, Oscar Joshua, Vincent Bossou, Mbuyu Twite, Kevin Yondan, Pato Ngonyani na Nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro'.
Viungo; Thabani Kamusoko, Salum Telela, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Deus Kaseke na Godfrey Mwashiuya.
Washambuliaji; Donald Ngoma, Matheo Anthony, Amissi Tambwe na Paul Nonga.
BENCHI LA UFUNDI;
Kocha Mkuu; Hans van der Pluijm (Uholanzi)
Kocha Msaidizi; Juma Mwambusi
Kocha wa makipa; Juma Pondamali
Daktari; Edward Bavu
Mchua Misuli; Jacob Onyango
Mtunza Vifaa; Mohammed Mpogolo
Meneja; Hafidh Saleh
WACHEZAJI WALIOBAKI DAR;
Benedicto Tinocco, Said Juma, Issoufou Boubacar na Malimi Busungu.
onthespottz.blogspot.com
Hao ni kipa Benedicto Tinocco ambaye hayumo kwenye programu za mchezo sawa na viungo Said Juma na Issoufou Boubacar, wakati Malimi Busungu ni majeruhi.
Yanga inatarajiwa kuondoka Saa 12:00 asubuhi ya kesho kwenda Angola kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa mchujo wa kuwania kutinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji Sagrada Esperanca Jumatano.
Katika mchezo huo, Yanga itahitaji hata sare kusonga mbele, baada ya awali kushinda 2-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, mabao ya Simon Msuva na Matheo Anthony.
![]() |
| Kocha wa Yanga SC, Hans van der Pluijm (kulia) akiwa na Waziri wa Kilimo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba |
Yanga imeangukia katika kapu la kuwania kucheza hatua ya makundi ya Shirikisho, baada ya kutolewa na Al Ahly ya Misri katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao 3-2, ikilazimishwa sare ya 1-1 Dar es Salaam na kufungwa 2-1 Alexandria.
Yanga ilianza vizuri tu kwa kuzitoa Cercle de Joachim ya Mauritius kwa jumla ya mabao 3-0, ikishinda 1-0 ugenini na 2-0 nyumbani kabla ya kuitoa na APR ya Rwanda kwa jumla ya mabao 3-2, ikishinda 2-1 Kigali na kutoa sare ya 1-1 Dar es Salaam.
Kwa upande wao, Sagrada Esperanca katika Raundi ya Awali waliitoa Ajax Cape Town ya Afrika Kusini kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya kufungwa 2-1 ugenini na kushinda 2-0 nyumbani. Katika Raundi ya kwanza wakaitoa LD Maputo ya Msumbiji kwa jumla ya mabao 2-1 ikishinda 1-0 nyumbani na kutoa sare ya 1-1 ugenini na kwenda hatua ya 16 Bora, ambako waliitoa V. Club Mokanda ya Kongo kwa jumla ya mabao 4-1 wakishinda 2-1 ugenini na 2-0 nyumbani.
Kila la heri na safari njema Yanga SC.
KIKOSI CHA YANGA KILICHOPO KIGALI;
Makipa; Ally Mustafa ‘Barthez’ na Deo Munishi ‘Dida’.
Mabeki; Juma Abdul, Mwinyi Haji, Oscar Joshua, Vincent Bossou, Mbuyu Twite, Kevin Yondan, Pato Ngonyani na Nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro'.
Viungo; Thabani Kamusoko, Salum Telela, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Deus Kaseke na Godfrey Mwashiuya.
Washambuliaji; Donald Ngoma, Matheo Anthony, Amissi Tambwe na Paul Nonga.
BENCHI LA UFUNDI;
Kocha Mkuu; Hans van der Pluijm (Uholanzi)
Kocha Msaidizi; Juma Mwambusi
Kocha wa makipa; Juma Pondamali
Daktari; Edward Bavu
Mchua Misuli; Jacob Onyango
Mtunza Vifaa; Mohammed Mpogolo
Meneja; Hafidh Saleh
WACHEZAJI WALIOBAKI DAR;
Benedicto Tinocco, Said Juma, Issoufou Boubacar na Malimi Busungu.
onthespottz.blogspot.com
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...




No comments: