Posted by On the spot Tz
10:12:00 PM
0
Sakata la uuzwaji kinyemela wa zaidi ya hekari 200 za shamba la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Mkoa wa Iringa limechukua sura mpya baada ya aliyekuwa katibu wa mkoa huo, Ally Nyawenga kukamatwa na polisi.
Shamba hilo lililopo eneo la Igumbiro, nje kidogo ya mji wa Iringa, linadaiwa kuuzwa mwaka jana kwa zaidi ya Sh800 milioni baada ya baadhi ya viongozi kubadili matumizi yake na kuwa viwanja.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, John Kauga alisema jana kuwa kiongozi huyo alikamatwa Morogoro siku chache zilizopita.
“Tulituma askari wetu na leo hii wanamleta. Taarifa za kumkamata ni hizo za uuzwaji wa shamba hilo kwa hivyo tutafanya naye mahojiano zaidi, lakini kwa sasa sina taarifa zaidi ya hapo labda tuwasiliane kesho (leo),” alisema.
Nyawenga alisimamishwa kazi mwishoni mwa mwaka jana, akituhumiwa kusimamia uuzwaji wa shamba hilo kinyume cha utaratibu wa jumuiya hiyo.
Mali zote za jumuiya hiyo zipo chini ya Baraza la Wadhamini, linaloongozwa na Mwenyekiti, Dk Emmanuel Nchimbi.
UVCCM ilianza kumiliki shamba hilo miaka ya 1970 likitumika kwa ajili ya kilimo kwa kukodisha vijana kwa bei nafuu ili kuwasaidia kujiendeleza kiuchumi.
Ally Simba aliyedaiwa kuwa msimamizi wa shamba hilo alikana nafasi hiyo huku akisema hakuhusishwa katika mipango hiyo.
“Sikuwa msimamizi, bali mjumbe tu wa kamati ya utekelezaji, msimamizi alikuwa Katibu wa UVCCM,” alisema Simba ambaye kwa sasa ni Katibu wa UVCCM Wilaya ya Mbinga.
Alisema kabla ya kuondoka Iringa mwaka 2014, hakuwahi kusikia vikao wala mipango ya uuzaji wa shamba hilo na kwamba hahusiki.
Akizungumzia kukamatwa kwa Nyawenga, Katibu wa UVCCM Mkoa wa Iringa, Abdulkarim Halamga alisema: “Kwa sababu ni mali ya vijana na katibu aliyekuwapo anahusika, hivyo kwa kushirikiana na polisi, tumemkamata baada ya waliouziwa viwanja kuanza kutudai huku vijana wakipinga kuuzwa kwa eneo lao. Kwa sababu hakuwa peke yake, taratibu nyingine zitafuatwa akishafikishwa Iringa.”
Mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya UVCCM mkoani hapo, Thom Muyinga alisema kuuzwa kwa shamba hilo kumesababisha mpasuko ndani ya umoja huo. “Vijana wanataka mali yao, haiwezekani mali hiyo iuzwe kinyemela na kunufaisha kundi la watu wachache,” alisema.
Mmoja wa vijana hao, Katula Kalinga alisema japo tayari tume ya UVCCM ya kuchunguza mgogoro huo ilishakwenda Iringa, hakuna kinachoendelea.
Alimuomba Rais John Magufuli kufuta hati za viwanja hivyo ili shamba hilo, lirejeshwe kwa UVCCM.
Pia, walimuomba Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete kutumbua majipu yanayokitafuna chama kwenye mkoa huo, ili vijana waendelee kunufaika na mali yao.
Walitaka kamati ya utekelezaji jumuiya hiyo Mkoa wa Iringa isimamishwe wakati uchunguzi ukiendelea.
onthespottz.blogspot.com
Shamba hilo lililopo eneo la Igumbiro, nje kidogo ya mji wa Iringa, linadaiwa kuuzwa mwaka jana kwa zaidi ya Sh800 milioni baada ya baadhi ya viongozi kubadili matumizi yake na kuwa viwanja.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, John Kauga alisema jana kuwa kiongozi huyo alikamatwa Morogoro siku chache zilizopita.
“Tulituma askari wetu na leo hii wanamleta. Taarifa za kumkamata ni hizo za uuzwaji wa shamba hilo kwa hivyo tutafanya naye mahojiano zaidi, lakini kwa sasa sina taarifa zaidi ya hapo labda tuwasiliane kesho (leo),” alisema.
Nyawenga alisimamishwa kazi mwishoni mwa mwaka jana, akituhumiwa kusimamia uuzwaji wa shamba hilo kinyume cha utaratibu wa jumuiya hiyo.
Mali zote za jumuiya hiyo zipo chini ya Baraza la Wadhamini, linaloongozwa na Mwenyekiti, Dk Emmanuel Nchimbi.
UVCCM ilianza kumiliki shamba hilo miaka ya 1970 likitumika kwa ajili ya kilimo kwa kukodisha vijana kwa bei nafuu ili kuwasaidia kujiendeleza kiuchumi.
Ally Simba aliyedaiwa kuwa msimamizi wa shamba hilo alikana nafasi hiyo huku akisema hakuhusishwa katika mipango hiyo.
“Sikuwa msimamizi, bali mjumbe tu wa kamati ya utekelezaji, msimamizi alikuwa Katibu wa UVCCM,” alisema Simba ambaye kwa sasa ni Katibu wa UVCCM Wilaya ya Mbinga.
Alisema kabla ya kuondoka Iringa mwaka 2014, hakuwahi kusikia vikao wala mipango ya uuzaji wa shamba hilo na kwamba hahusiki.
Akizungumzia kukamatwa kwa Nyawenga, Katibu wa UVCCM Mkoa wa Iringa, Abdulkarim Halamga alisema: “Kwa sababu ni mali ya vijana na katibu aliyekuwapo anahusika, hivyo kwa kushirikiana na polisi, tumemkamata baada ya waliouziwa viwanja kuanza kutudai huku vijana wakipinga kuuzwa kwa eneo lao. Kwa sababu hakuwa peke yake, taratibu nyingine zitafuatwa akishafikishwa Iringa.”
Mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya UVCCM mkoani hapo, Thom Muyinga alisema kuuzwa kwa shamba hilo kumesababisha mpasuko ndani ya umoja huo. “Vijana wanataka mali yao, haiwezekani mali hiyo iuzwe kinyemela na kunufaisha kundi la watu wachache,” alisema.
Mmoja wa vijana hao, Katula Kalinga alisema japo tayari tume ya UVCCM ya kuchunguza mgogoro huo ilishakwenda Iringa, hakuna kinachoendelea.
Alimuomba Rais John Magufuli kufuta hati za viwanja hivyo ili shamba hilo, lirejeshwe kwa UVCCM.
Pia, walimuomba Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete kutumbua majipu yanayokitafuna chama kwenye mkoa huo, ili vijana waendelee kunufaika na mali yao.
Walitaka kamati ya utekelezaji jumuiya hiyo Mkoa wa Iringa isimamishwe wakati uchunguzi ukiendelea.
onthespottz.blogspot.com

Tagged with:
HABARI KITAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: