Posted by On the spot Tz
2:35:00 AM
0
Umoja wa Mataifa umesema kuwa, kitendo cha Sudan cha kukataa kumuongezea muda wa iqama na kibali cha kuishi afisa mmoja wa ngazi za juu wa umoja huo, kina maana ya kumfukuza nchini humo.
Shirika la habari la Ufaransa jana lilinukuu taarifa ya umoja huo ikisema kuwa, serikali ya Sudan imekataa kumuongezea muda wa iqama Ivo Freijsen, mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya uratibu wa misaada ya kibinadamu. Umoja wa Mataifa ulikuwa umeiomba Khartoum imwongezee afisa wake huyo muda wa miezi 12 mingine wa kuishi Sudan. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, hatua hiyo ya Khartoum ni uvunjaji wa hati na makubaliano ya Umoja wa Mataifa.
Freijsen ambaye tangu mwezi Februari 2014 amekuwa mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya uratibu wa misaada ya haki za binadamu nchini Sudan, ni afisa wa nne wa ngazi za juu wa umoja huo kufukuzwa nchini humo katika kipindi cha miaka miwili iliiyopita.
Wakala mmoja wa uratibu wa masuala ya kibinadamu unaoundwa na mashirikia ya Umoja wa Mataifa na taasisi nyingine nyingi zisizo za kiserikali zimeelezea kusikitishwa kwao na hatua ya serikali ya Sudan ya kumfukuza afisa huyo mwandamizi wa Umoja wa Mataifa.
Afisa huyo amefukuzwa nchini Sudan miezi michache tu tangu nchi hiyo ifunge ofisi ya shirika lisilo la kiserikali la Tearfund na kuwafukuza viongozi watatu wa shirika hilo katika miezi ya hivi karibuni..

Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: