Posted by On the spot Tz
12:21:00 AM
0
BEKI wa Liverpool, Mamadou Sakho katika mazingira ya kustaajabisha ameruhusiwa kuichezea Ufaransa kwenye Fainali za Euro 2016 baada ya UEFA kuamua kusitisha kwa muda adhabu ya kufungiwa kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Kocha wa Ufaransa, Didier Deschamps sasa ana saa 72 za kuamua kumjumuisha Sakho kwenye kikosi chake au kufuatia kuumia kwa Raphael Varane wa Real Madrid.
Vikosi vyote vya Euro 2016 vinatakiwa kuwa vimewasilishwa hadi kufika Mei 31, ingawa kujumuishwa kwa Sakho kutazua utata baada ya kugundulika kutumia dawa za kuongeza nguvu zilizopigwa marufuku michezoni Machi 17.
Mamadou Sakho
Awali Sakho alifungiwa siku 30 Aprili 28 kufuatia vipimo alivyofanyiwa baada ya mchezo wa Europa League dhidi ya Manchester United kuthibitisha alitumia dawa hizo.
Adhabu hiyo inamalizika Jumamosi na UEFA imeshindwa kupiga hatua zaidi baada ya Sakho kuwasilisha utetezi wake Jumatatu.
Timu ya utetezi wa Sakho iliwasilisha vielelezo vya kisayansi katika kesi hiyo na UEFA imeiagiza Kamati yake Nidhamu kwanza kuchunguza zaidi kabla ya hatua kuchukuliwa.
Na baada ya adhabu yake ya awali kusitishwa, kwa sasa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, Sakho anaweza kujumuishwa kwenye kikosi cha Les Bleus

Tagged with:
MICHEZO KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: