Posted by On the spot Tz
10:38:00 PM
0
Kocha Wa Azam : Stewart Hall
AZAM FC imekatwa pointi tatu na mabao matatu iliyovuna katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Mbeya City Februari 20, mwaka huu Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
Hiyo inafuatia madai ya kumtumia beki Erasto Edward Nyoni katika mchezo akiwa ana kadi tatu za njano.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas Mapunda amesema kwamba pamoja na kupokwa pointi hizo, benchi la Ufundi la Azam FC limepewa onyo kuwa makini na taarifa za wachezaji wake.
Kwa kukatwa pointi hizo, Azam FC sasa inabakiwa na pointi 57 baada ya kucheza mechi 27 na kuporomoka kwa nafasi moja hadi ya tatu, wakiipisha Simba SC yenye pointi 58 za mechi 26, huku Yanga yenye pointi 68 za mechi 27 ikiendelea kuongoza ligi hiyo.
Katika hatua nyingine, kocha wa Azam FC Muingereza Stewart John Hall amesem ataondoka katika klabu hiyo baada ya kumaliza msimu.
Stewart amesema anamalizia mechi tatu za Ligi Kuu na Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Kombe la Azam Sports Federation (ASFC) na baada ya hapo ataondoka.
onthespottz.blogspot.com

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: