Posted by On the spot Tz
12:49:00 PM
0
Jackson Mayanja
Uongozi wa Simba, umeanza kazi kimyakimya ya kufanya mazungumzo na makocha kadhaa wa nje ya Tanzania.
Taarifa zinaeleza, uongozi wa Simba unataka kuimarisha benchi lake la ufundi kwa kusajili makocha wenye uwezo wa juu.
“Kweli hiyo kazi imeanza, lakini hatuwezi kusema ni kutoka wapi na itakuwaje,” kilieleza chanzo.
Taarifa nyingine zinaeleza kwamba Simba imeanza maandalizi pia ya kumpata kocha mpya wa makipa.
“Ninavyojua viongozi wa Simba wameamua kufanya mambo yao kimyakimya kwanza. Wanachunguza lakini watakachofanya kikubwa ni kuboresha benchi la ufundi.”
Kocha Jackson Mayanja raia wa Uganda, alijiunga na Simba katika nafasi ya kocha msaidizi lakini kabla ya kuanza kazi, aliyekuwa Kocha Mkuu, Dylan Kerr akatimuliwa.
Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments: