Posted by On the spot Tz
1:37:00 PM
0
Serengeti Boys wameonyesha wanaweza kweli baada ya kuwaonyesha soka wenyeji India kwa kuwachapa mabao 3-1 katika mechi ya michuano ya vijana ya AIFF inayoendelea mjini Goa.
Boys walioonyesha soka safi ndiyo walikuwa wa safi walifanikiwa kupata bao kupitia kwa Maziku Amani katika dakika ya 20.
Maziku tena aliunganisha mpira na kuandika bao la pili katika dakika ya 28 na kuwaduwaza wenyeji.
Baadaye India walionekana kuamka na kufanikiwa kupata bao katika dakika ya 36 kupitia Komal Thatal na hadi mapumziko ikawa 2-1.
Kipindi cha pili, vijana hao wa Tanzania ndiyo walionyesha soka bomba zaidi na kufanikiwa kupata bao jingine katika dakika ya 47, mfungaji akiwa Asad Ali.
Baada ya hapo, Boys walionekana kuuchezea zaidi mpira, wakipiga pasi za uhakika na kuwakatisha tamaa kabisa wenyeji hao ambao wana kikosi chao kilichotengenezwa chini ya uangalizi bora kwa zaidi ya miaka mitano.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
WATOTO WA KAGAME WAITIKISA TIMU YA TAIFA YA RWANDA,,,,,,Kwa mara ya Kwanza wanawe rais wa Rwanda Paul Kagame, Bryan Kagame na Ian Kagame waliiwakilisha timu ya taifa ya Rwanda kwa wachezaji wasi...
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
UCHAGUZI MAREKANI WAPAMBA MOTO,,,,,Wagombea Urais marekani Licha ya ushindi wa Trump wa Jumanne ya jana kuzidi kumuhak...
No comments: