Posted by On the spot Tz
2:44:00 PM
0

Timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti Boys wamepata sare nyingine baada ya Malaysia kusawazisha mabao yote mawili waliyotangulia kufunga vijana hao.
Mechi hiyo ni ya michuano ya Kombe la Vijana la AIFF inayofanyika katika mji wa Goa nchini India.
Boys walianza kupata bao lao la kwanza katika dakika ya 31 kupitia mshambuliaji wao hatari, Asad Ali Juma na Yohana Oscar akaongeza la pili katika dakika ya 59, ikiwa ni dakika chache baada ya kuanza kwa kipindi cha pili.
Makosa ya walinzi, yaliwaruhusu Malaysia kusawazisha mabao yote mawili ndani ya dakika tano tu.
Walianza kupata bao la kwanza katika dakika ya 63 kupitia Arif Suhaimi na Najmi Idhar akafunga la pili katika dakika ya 68.
Hii ni sare ya tatu kwa Boys zikiwemo zile za 1-1 dhidi ya Marekani, 2-2 dhidi ya Korea na imepata ushindi mmoja wa mabao 3-1 dhidi ya wenyeji India. Inaendelea kuwa haijapoteza hata mechi moja katika michuano hiyo.
Tagged with:
MICHEZO KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: