Posted by On the spot Tz
9:26:00 AM
0
Polisi nchini Kosovo imemtia mbaroni kasisi mmoja wa Kanisa Katoliki anayedaiwa kuwanajisi watoto wadogo katika taasisi moja ya kidini nchini Uingereza na kisha kutoroka nchi.
Veton Elshani, Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Ushirikiano wa Kimataifa cha Kosovo amesema kasisi huyo wa Uingereza kwa jina Andrew Charles Kingston Soper alikamatawa akiwa mafichoni katika mji wa Peja, mashariki mwa nchi. Amesema kuwa kasisi huyo amekamatwa kutokana na waranti iliyotolewa na serikali ya London mwaka 2011.
Idara ya Mashtaka ya Umma nchini Kosovo imeagiza kuendelea kuzuiliwa kasisi huyo mtoro hadi mahakama ya nchi hiyo iamue iwapo atarejeshwa nchini Uingereza au la.
Kingston Soper ambaye pia anafahamika kama Father Laurence, anadaiwa kuwanajaisi watoto watano ambao walikuwa wanafunzi wake katika shule binafsi inayomilikiwa na Kanisa Katoliki ya St. Benedict’s, katika kitongoji cha Ealing Abbey magharibi mwa mji mkuu wa Uingereza, London.
Haya yanajiri siku chache baada ya Dayosisi Kuu ya Kanisa Katoliki katika mji wa Baltimore jimboni Maryland nchini Marekani kufichua majina ya makasisi 71 wanaotuhumiwa kuwalawiti watoto wadogo.
Kwa mujibu wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini Marekani, takriban makasisi 6,900 wa Kanisa Katoliki la Roma wanadaiwa kuwalawiti watoto wadogo 16,900 kati ya mwaka 1950 na 2011.
Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: