Posted by On the spot Tz
2:06:00 PM
0
Mwanamke mmoja nchini India amejifungua mtoto wa uzani wa kilo 6.8 ambaye madaktari wanasema huenda akawa mtoto mwenye uzani wa juu zaidi kuwahi kuzaliwa nchini humo.
Mtoto huyo ana uzani sawa na mtoto wa umri wa miezi sita.
Nchini humo, watoto huzaliwa na uzani wa kadiri wa kilo 2.5-3.5.
Mamake Nandini, 20, alijifungua kupitia upasuaji katika jimbo la Karnataka, kusini mwa nchi hiyo.
Afisa wa afya wa hospitali ya wilaya ya Hassan, Dkt Venkatesh R, ameambia BBC kwamba mtoto huyo pia ni mrefu wa kimo.
Mtoto huyo ana kimo cha sentimeta 62 (inchi 24.4in) ilhali kwa kawaida watoto India huzaliwa na kimo cha sentimeta 50,"amesema Dkt SR Kumar, anayemtunza Nandini na mwanawe.
Visa vya watoto kuzaliwa na uzani wa juu kupindukia sana hutokana na mama kuugua kisukari lakini madaktari wamebaini Nandini hana tatizo hilo.
Rekodi ya mtoto mwenye uzani wa juu zaidi India inashikiliwa na mvulana aliyezaliwa na Firdous Khatun jimbo la Uttar Pradesh Novemba 2015. Mvulana huyo alikuwa na uzani wa kilo 6.7.
Rekodi ya dunia inashikiliwa na mvulana aiyezaliwa na Carmelina Fedele eneo la Aversa, Italia, mwezi Septemba 1955. Alikuwa na uzani wa kilo 10.2.
onthespottz.blogspot.com
Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Shilingi Bilioni 3 na Mali za Bilioni 10 zataifishwa na TRA Kutoka kwa Wakwepa Kodi Bandari Kavu ya Azam,,,,,,,Mamlaka ya kukusanya kodi TRA kupitia madalali wa Yono Auction Mart wamekusanya mali za bilioni 3 pamoja na kutaifisha mali za b...


No comments: