Posted by On the spot Tz
4:13:00 AM
0
Leo Manchester United wanavaana na Crystal Palace katika mchezo wa fainali ya kombe la FA utakaopigwa kwenye uwanja wa Wembley.
United hawakuwa na msimu mzuri baada kuishia hatua ya makundi UEFA na kudondokea michuano ya EUROPA ambayo hata hivyo walitupwa nje na Liverpool, hivyo kombe la FA ni muhimu sana kwao ili kufuta machozi ya machungu waliyopata.
United pia wamekosa nafasi ya kufuzu kucheza UEFA mwakani baada ya kushika nafasi ya tano nyuma ya Leicester, Arsenal, Tottenham na Manchester City.
Hata hivyo wakati United ikiwa chini ya Sir Alex Ferguson, kombe la FA lilikuwa kama ziada tu hasa baada ya kuibuka mabingwa wa ligi kuu, ukizingatia ya kwamba walikuwa wakishinda mara kadhaa kwa pamoja ubingwa wa ligi kuu na makombe mengine likiwemo FA.
Hivyo basi, United wameamua kwamba endapo watashinda ubingwa wa FA leo, kamwe hawatafanya ‘bus parade’ kwenye jiji la Manchester kwa kuwa si kitu chenye uzito mkubwa kwao.
Bus parade hufanywa na timu zinazochukua makombe mbalimbali ikiwa ni maalum kwa ajili ya kuwaonyesha mashabiki kombe/makombe waliyochukua.
Tagged with:
MICHEZO KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Shilingi Bilioni 3 na Mali za Bilioni 10 zataifishwa na TRA Kutoka kwa Wakwepa Kodi Bandari Kavu ya Azam,,,,,,,Mamlaka ya kukusanya kodi TRA kupitia madalali wa Yono Auction Mart wamekusanya mali za bilioni 3 pamoja na kutaifisha mali za b...



No comments: