Licha  Ya  Manyika,Agban  Simba  Yasaka Kipa Mpya,,,

                                                                    MANYIKA  JR

                                                         VICENT  AGBAN

Klabu ya Simba imeanza kusaka kipa mwingine mzoefu kwa ajili ya kujiimarisha kwa msimu ujao.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba, zimeeleza tayari juhudi za kumnasa kipa mpya zimeanza.
“Kipa kweli anatafutwa, Manyika na Agbani pia watabaki. Lengo ni kutanua zaidi wigo katika nafasi ya ulinzi wakianzia na kipa.

“Kipa anayetafutwa anatakiwa kuwa wa humu Tanzania. Halafu Agbani yeye ataendelea kubaki,” kilieleza chanzo.


Kwa msimu wote, Simba zaidi imewatumia makipa wawili, Vicent Agbani raia wa Ivory Coast na Peter Manyika ambaye zaidi alidaka mechi za mwanzoni na sasa mwishoni amekuwa akipewa nafasi.
onthespottz.blogspot.com

«
Next

Newer Post

»
Previous

Older Post


No comments:

Leave a Reply