Posted by On the spot Tz
1:36:00 PM
0
Jamhuri kihwelo "julio"
Kocha Mkuu wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amemtangaza kuwa kocha bora wa Tanzania.
Julio amesema hayo mara tu baada ya mechi kati yao dhidi ya Simba kwisha na Mwadui FC kushinda kwa bao 1-0.
“Mimi ndiye kocha bora hapa Tanzania. Nilitaka sana kuifunga Simba ili kuwaonyeshea kuwa mimi ninaweza kuwafunga kwa kuwa nina uwezo.
“Hawa Simba walitufukuza mimi na kocha Kibadeni, hii ni laana yetu kwa kuwa nilianza kumfunga kocha wao wa zamani (Patrick Liewig wa Stand United). Leo nimewafunga tena leo kupitia kocha wao sijui nani, sijui Mayanja.
“Nataka wajue makocha wazalendo pia wanapaswa kuthaminiwa. Waache mambo yao ya kizamani kuwa wanaona makocha wazalendo hawana maana. Waache majungu, waache kutudharau,” alisema Julio akionyesha kujiamini.
KIkosi cha Mwadui kilionyesha soka safi na kuizidi Simba ambayo licha ya kucheza vizuri lakini ilishindwa kuonyesha kuwa ingeifunga Mwadui FC.

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: