Posted by On the spot Tz
1:38:00 PM
0
KIUNGO chipukizi wa Azam FC, Omar Wayne amefaulu majaribio katika klabu ya AmaZulu ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini, lakini kutokana na umri wake mdogo wa miaka 18 ameambiwa akaanzie timu B.
Akizungumza jana kutoka Durban, Wayne amesema kwamba AmaZulu wamemuambia akaanzie timu B ili apate uzoefu zaidi.
Hata hivyo, Wayne amesema kwamba kwa kuwa timu B atakuwa amesaini Mkataba wa soka ya ridhaa hana uhakika kama Azam FC itamuachia bure.
“Kwanza timu B maana yake hawa hawawezi kuilipa Azam, sasa na mimi nina Mkataba na Azam, sijui itakuwaje…ila nimewaambia sasa wakasema wanakwenda kufanya kikao, nasubiri majibu ya kikao chao,”alisema Wayne jana.
![]() |
Omar Wayne akiwa kwenye chumba cha kubadilishia nguo cha AmaZulu jana |
Katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu, Wayne alihamia Coastal Union pia kwa mkopo ambako wiki mbili zilizopita aliondoka kwenda Afrika Kusini kufanya majaribio.
Wakala Rogers wa Afrika Kusini alivutiwa na Wayne baada ya kumuona akiichezea timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Tanzania, Serengeti Boys dhidi ya U17 ya Afrika Kusini mwaka jana.
Pamoja na Serengeti kutolewa, lakini soka ya Wayne iliwavutia wengi na tangu hapo wamekuwa wakimfuatilia kabla ya kupewa nafasi ya majaribio ya kucheza Afrika Kusini.
![]() |
Wayne na Ibrahim Hajib wamekutana mjini Durban na wote wako chini ya Rodgers |
Mbali na Wayne, mchezaji mwingine wa Tanzania ambaye kwa sasa yupo kwenye majaribio Afrika Kusini ni mshambuliaji Ibrahim Hajib wa Simba ambaye leo anatarajiwa kuanza majaribio Golden Arrows pia ya Ligi Kuu ya nchi hiyo.
Ni mchezaji mmoja tu ambaye inafahamika anacheza Ligi Kuu ya ABSA ya Afrika Kusini, Mrisho Khalfan Ngassa wa Free State Stars.
onthespottz.blogspot.com

Tagged with:
MICHEZO KITAIFA.
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mashabiki na Wanachama wa Yanga Wachoma Magazeti Yanayomilikiwa na Reginald Mengi.,,,,,,Wanachama na mashabiki wa Yanga leo wakiyachana na kuyachoma moto magazeti ya The Guardian na Nipashe yanayomilikiwa na kampuni ya IPP MED...
No comments: