Posted by On the spot Tz
12:45:00 AM
0
Kikosi cha kusimamia amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM kikishirikiana na kikosi cha serikali ya Mogadishu vimefanikiwa kuyakomboa maeneo mengi yaliyokuwa chini ya udhibiti wa wanamgambo wa al-Shabab.
Ripoti kutoka Somalia zinasema kuwa, vikosi hivyo vimepata mafanikio katika operesheni zao za hivi karibuni dhidi ya wanamgambo wa al-Shabab na kuyakomboa maeneo mengi yaliyokuwa chini ya udhibiti wa wanamgambo hao.
kwa mujibu wa maafisa wa kijeshi wa AMISOM ni kuwa, wanamgambo wa al-Shabab wamelazimika kuondoka katika maeneo mengi yaliyokuwa ni ngome zao kutokana na kuandamwa na operesheni ya pamoja ya kijeshi dhidi yao.
Kikosi cha kusimamani amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM kinachoundwa na nchi za Kenya, Ethiopia, Uganda na Burundi kimekuwa nchini Somalia tangu mwaka 2007.
Licha ya mafanikio hayo ya AMISOM na kikosi cha serikali ya Somalia, lakini wanamgambo wa al-Shabab wangali wanatekeleza mashambulio ya hapa na pale katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo na kusababisha mauaji ya watu.
Ikumbukwe kuwa, askari 15 wa Somalia waliuawa katika shambulio la jana la wanamgambo wa al-Shabab katika mji wa Runirgood kaskazini mashariki mwa mji mkuu Mogadishu.
Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Kiongozi wa Upinzani Uganda Besigye Ashtakiwa Kwa Uhaini,,,Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hiv...
-
HARRY KANE ATWAA KIATU CHA DHAHABU ENGLAND,,,,,,,Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Harry Kane akiwa na picha hya kiatu cha dhahabu cha Ligi Kuu ya Enfland baada ya kiibuka mfungaji bora...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...


No comments: