Posted by On the spot Tz
9:00:00 PM
0
Polisi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imewashambulia waandamanaji waliokuwa wanaandamana kupinga kuahirishwa tarehe ya uchaguzi mkuu wa nchi hiyo.
Katika hujuma hiyo polisi wametumia mabomu ya kutoa machozi sanjari na kuwatia mbaroni baadhi ya waandamanaji hao. Jean-Bosco Kalenga afisa wa ngazi za juu katika kikosi cha polisi amedai kuwa, polisi iliwashambulia waandamanaji hao kwa kuwa walikuwa wanahatarisha usalama wa nchi. Katika mji wa Lubumbashi, kusini mashariki mwa nchi hiyo, polisi pia imewashambulia waandamanaji wanaokadiriwa kufikia 5000, ambao walimiminika mabarabarani kupinga hatua hiyo ya kusogezwa mbele tarehe ya uchaguzi mkuu uliokuwa umepangwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu. Waandamanaji walikusanyika mbele ya ofisi za Muungano wa Kitaifa wa Kifederali UNAFEC, za wapinzani wa serikali ya Rais Joseph Kabila. Kabla ya hapo, viongozi wa upinzani walikusanyika mbele ya ofisi za muungano huo mjini Kinshasa na kulaani hatua za rais huyo zilizo kinyume na demokrasia. Kwa sasa anga ya kisiasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imekuwa tete kufuatia hatua ya kamisheni huru ya uchaguzi ya nchi hiyo kuahirisha uchaguzi mkuu, hatua ambayo inatajwa kuwa ni njama za kumsafishia njia Rais Kabila ya kuendelea kusalia madarakani. Kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo, Rais Joseph Kabila aliyeingia madarakani mwaka 2001, haruhusiwi tena kugombea uchaguzi ujao
Tagged with:
KIMATAIFA
On the spot Tz
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
-
Makahaba Dar es Salaam Wamzidi Nguvu Paul Makonda,,,,,,,,,Ving’ang’anizi! Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda la kuwataka akina dada wanaouza miili ‘makahaba’ kuondoka kwenye ‘mas...
-
Mwingine Adakwa Kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kwenye Mtandao wa "WhatsApp",,,,,,,Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais ...
-
Old Trafford Kwategwa Bomu Hewa,,,Mashabiki wapatao 20,000 wametolewa nje kwenye Uwanja wa Old Trafford na kusababisha kuchelewa kuanza kwa mechi katyi ya Manchester Uni...
-
Shilingi Bilioni 3 na Mali za Bilioni 10 zataifishwa na TRA Kutoka kwa Wakwepa Kodi Bandari Kavu ya Azam,,,,,,,Mamlaka ya kukusanya kodi TRA kupitia madalali wa Yono Auction Mart wamekusanya mali za bilioni 3 pamoja na kutaifisha mali za b...


No comments: